Simba yaiziba mdomo Pamba Jiji
Timu ya Simba jioni ya leo imeibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Pamba Jiji katika muendelezo wa Ligi Kuu bara katika uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza.
Mabao ya Simba yalifungwa kipindi cha kwanza na Clatous Chama na Anicet Oura wakati goli la kufuatia machozi la Pamba limefungwa kwa mkwaju wa penati iliyotibua ‘clean-sheet’ kwa Simba; Idrisa Diomande.
Kwa matokeo hayo Simba insfikisha pointi 6 na kukaa kileleni baada ya kucheza mechi mbili.
