Simba SC chapa bora Tanzania
Klabu ya Simba SC imeendelea kudhihirisha ukubwa na uthabiti wa chapa yake baada ya kutunikiwa rasmi cheti cha Superbrand kama taasisi namba moja inayojihusisha na michezo nchini Tanzania kwa mwaka wa pili mfululizo.
Tuzo hii inadhihirisha ukuaji mkubwa wa thamani ya chapa (brand) ya Msimbazi, ubora wa utendaji wa kitaasisi, pamoja na ushawishi wake mkubwa katika sekta ya michezo nchini na barani Afrika.



