Rais Samia awatakia kheri ya Maulid
Ninawatakia Waislamu na Watanzania wote kheri na baraka za Sikukuu ya Maulid. Kumbukizi ya siku hii njema ya kuzaliwa kwa Mtume Muhammad (S.A.W) itukumbushe kuendelea kuishi kwa upendo, huruma, uvumilivu na kuwajali wengine.
Tusherehekee kwa amani na furaha, huku tukidumisha umoja na mshikamano wetu. Mwenyezi Mungu Mtukufu aendelee kuibariki nchi yetu, kuitunza katika amani na utulivu, na kutuwezesha kuijenga kwa maendeleo na ustawi wa wote.
Mawlid Al Nabi Mubarak.
