Patrick Vieira awa kocha mkuu Senegal

Shirikisho la Soka la Senegal (FSF) limemtangaza rasmi Patrick Vieira kuwa kocha Mkuu wa Timu ya taifa ya Senegal

Vieira, ambaye ni gwiji wa soka la kimataifa na aliyekuwa akiichezea timu ya taifa Ufaransa, alizaliwa jijini Dakar, Senegal.

Uteuzi huo unamfanya Vieira kurejea nchini alikozaliwa akiwa na jukumu la kuiongoza timu ya taifa ya Senegal.

Patrick amesaini mkataba wa miaka minne akichukua nafasi ya Pape Thiaw aliyeondoka mwezi uliopita.


Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

Kocha Simba anataka wachezaji wapya watano

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI