Okello aanika mshahara wake, ni kufuru
Aliyekuwa kiungo mshambuliaji wa Yanga SC, Allan Okello, amevunja ukimya na kuaga rasmi klabu hiyo baada ya kuitumikia kwa muda mfupi lakini wenye mafanikio.
Katika ujumbe wake wa kwaheri, nyota huyo raia wa Uganda ametoa shukrani za dhati kwa uongozi wa Yanga SC chini ya Rais wa klabu, wachezaji wenzake, pamoja na mashabiki wa Wananchi kwa kumfanya ajisikie yupo nyumbani Tanzania, huku akisisitiza kuwa imekuwa heshima kubwa kwake kuvaa jezi ya kijani na njano.
Mara baada ya kuaga Wananchi, Okello amekamilisha usajili wa kujiunga na miamba ya soka nchini Morocco, klabu ya AS FAR (FAR Rabat), ambapo amesaini mkataba wa miaka mitatu kuanza changamoto mpya ya soka barani Afrika Kaskazini.
Hatua hii inamfanya kiungo huyo wa kimataifa wa Uganda kuanza maisha mapya katika Ligi Kuu ya Morocco (Botola Pro) akiwa miongoni mwa wachezaji kutoka Afrika Mashariki waliopata fursa ya kujiunga na klabu hiyo kubwa.
Usajili huu unakuja na maslahi makubwa ya kifedha ambapo Okello atakua akilipwa jumla ya Shilingi Milioni 445 za Kitanzania ($167,000) kwa mwaka.
Mchanganuo huo unamfanya kuingiza takribani Shilingi Milioni 37 kwa mwezi, sawa na Shilingi Milioni 8.5 kwa wiki na takribani Shilingi Milioni 1.2 kila siku. Je, unauonaje usajili huu wa Allan Okello kwenda Morocco na mshahara anaokwenda
