Mfungaji bora NBC Primier huyoo Algeria

KAMA ilivyoripotiwa na Mwanaspoti siku chache zilizopita, mshambuliaji wa kimataifa wa Burundi, Mossi Nduwumwe, amekamilisha rasmi uhamisho wake kutoka Singida Black Stars kwenda kwa mabingwa wa Algeria, MC Alger.

Awali, Mwanaspoti ilifichua kuwa Mossi alikuwa katika hatua za mwisho za kujiunga na MC Alger baada ya mazungumzo kati ya klabu hizo kufikia pazuri huku zikisalia taratibu chache za kukamilisha dili hilo.

Sasa taarifa hizo zimethibitishwa rasmi baada ya MC Alger kumtambulisha nyota huyo kupitia kurasa zake rasmi za mitandao ya kijamii.

Klabu hiyo ilimkaribisha mshambuliaji huyo kwa ujumbe wa "Welcome to Mouloudia", ikithibitisha kumalizika kwa moja ya usajili uliokuwa ukifuatiliwa kwa karibu baada ya kiwango bora alichoonyesha akiwa Singida Black Stars msimu uliopita.


Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

Kocha Simba anataka wachezaji wapya watano

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI