Injinia Hersi aikabidhi jezi ya Yanga familia ya Kifukwe
Rais wa Yanga, Hersi Said amekabidhi Jezi za Young Africans Sports kwa familia ya Rais wa zamani wa Yanga Francis Kifukwe, ikiwa ni ishara ya heshima na kutambua mchango mkubwa wa Baba yao kwenye klabu ya Yanga kipindi cha uongozi wake.
-
Mwili wa Kifukwe aliyefariki Jumamosi akiwa matibabu nchini India unaagwa mchana huu kwenye Ukumbi wa Karimjee, Dar es Salaam na utazikwa Jumamosi wiki hii yumbani kwao Kyela, Mbeya. (Picha kwa hisani ya Yanga SC).

