Doumbia aendelea kucheka na nyavu, ikiiua El Marreikh 2-0
Klabu ya Simba imeibuka na ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya El Merreikh ya Sudan katika mchezo wa kirafiki uliochezwa Kigali, Rwanda.
Simba imepata mabao yake kupitia kwa Libasse Gueye aliyefunga bao la kwanza, kabla ya Ibrahim Doumbia kuongeza la pili na kuipa timu hiyo ushindi.
Hii ni mara ya pili kwa straika huyo mpya wa Simba kucheka na nyavu ambapo mara ya kwanza alitupia wakati Simba ilipocheza na Singida BS kwenye Kagame CECAFA Cup

