Al Hilal yafanya balaa kubwa Rwanda
Miamba ya Sudan, Al Hilal Omdurman, imeendelea kuthibitisha umahiri wake mkubwa kwenye sekta ya usajili baada ya kuikanda Kiyovu Sports mabao 5-0 nchini Rwanda, huku nyota wao mpya Ansumana Samura akiwa mwiba mchungu dimbani!
Kijana huyo mwenye umri wa miaka 18 pekee, aliyekabidhiwa jezi ya aliyekuwa nyota wa timu hiyo Jean Girumugisha, ametia kambani mabao matatu na kuonyesha mwanzo wa kishindo.
Mabao mengine ya Al Hilal yaliwekwa kambani na Qamardine pamoja na Ahmed Salem kusaidia kukamilisha ushindi huo mnono wa mabao 5-0.
