Yanga Princess yaachana na Sportpesa

Timu ya Yanga Princess haitaitangaza tena kampuni ya kubashiri SportPesa. Hii ni kutokana na uamuzi wa timu hiyo kutafuta mdhamini wake wa kujitegemea, tofauti na ilivyokuwa awali ambapo udhamini wa timu ya wanaume ulihusisha pia timu ya wanawake.

Kuanzia sasa, wachezaji watakaotambulishwa hawatakuwa na tangazo lolote la SportPesa—iwe kwenye jezi za mazoezi, jezi za mechi, au mavazi yao mengine yote.

Yanga Princess sasa ipo kwenye mchakato wa kutafuta mdhamini mpya, na pia inakaribisha makampuni mbalimbali kujitangaza kupitia timu ya wanawake ya Yanga Princess.

Huu ni wakati wa mapinduzi—tuanze kuzipa thamani timu zetu za wanawake kwa kujitegemea katika udhamini, ili kuongeza hadhi yao na kupunguza mzigo wa kifedha ndani ya vilabu vyetu.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI