Ruka hadi kwenye maudhui makuu

SIMBA KUWAAGA BOCCO, MKUDE NI DHIHAKA AU MAPENZI

Na Prince Hoza Matua 

SEPTEMBA 10 klabu ya Simba SC inaadhimisha tamasha lake ya Simba Day katika uwanja wa Mkapa jijini Dar es Salaam, katika siku hiyo Wekundu wa Msimbazi watacheza mechi ya kirafiki na timu ya Police FC ya Kenya.

Police FC ni mabingwa wa nchi hiyo na watawakilisha taifa hilo katika michuano ya Ligi ya mabingwa Afrika kama ilivyo kwa Simba SC ambao wamemaliza nafasi ya pili kwenye Ligi Kuu bara msimu uliopita.

Katika tamasha hilo Simba SC watatumia nafasi hiyo ya kutambulisha jezi mpya, wachezaji wa kikosi chake cha msimu ujao na pia safi yake yote ikiwemo makocha.

Simba SC pia watatambulisha vikosi vyake vya timu za vijana kwa maana under-17 na under-20 pia timu ya wanawake, Simba Queens ambayo nayo imefanya usajili mkubwa kama ilivyo timu ya wanaume.

Kitu ambacho kinanifanya niandike makala hii ni kitendo cha klabu hiyo kuwaaga wachezaji wake wawili wa zamani wote wakiwa manahodha, John Raphael Bocco na Jonas Gelard Mkude.

Wachezaji hao waliichezea Simba kwa mafanikio makubwa lakini baadaye wakaachana na klabu hiyo na kutimkia vilabu vingine, Mkude yeye alidumu Simba misimu 13 na alijiunga Yanga SC ambao ni mahasimu wakuu wa Simba.

Na Bocco naye alidumu Simba misimu 8 na alitimkia JKT Tanzania, lakini uongozi wa Simba uliona umuhimu wa kuwapa heshima wachezaji hao na katika tamasha la Simba Day la mwaka huu wanawaaga rasmi.

Meneja wa Habari na mawasiliano Wa Klabu ya Simba SC Ahmed Ally amefunguka na kuthibitisha kuwa kwenye tamasha la Simba Day la mwaka huu itakuwa ni siku pia ya kuwaaga nyota wao wawili wa zamani wa kikosi hicho ambao ni Jonas Mkude na John Bocco.

Kwa ajili ya kutambua mchango wao ndani ya klabu hiyo ,huku pia akieleza kuwa mchezaji mwingine ambaye mashabiki wanamsubiri ataaagwa akimaliza pensheni yake japo hajataka kutaja jina lake.

"Tumeandaa utaratibu maalum wa kuwaaga wachezaji wetu vipenzi ambao waliitumikia Simba kwa muda mrefu lakini hatukupata bahati ya kuwaaga lakini niwaambie tumeshaongea nao na wamethibitisha watakuwepo Simba Day hii"
.
"Hapa namzungumzia John Bocco na Jonas Mkude  ambao walikaa Simba kwa muda mrefu lakini wakaondoka bila Kuagwa,  nitumie fursa hii kuwaambia kuwa Simba Day hii  itakuwa ni siku maalum ya kuwaaga wachezaji hawa", alisema Ahmed Ally.

Bila shaka tamasha la Simba Day lakuvutia sana kutokana na utofauti wake lakini mimi binafsi nashindwa kuwaelewa Simba SC kama wameamua kufanya tamasha hili na kuwaaga wachezaji hao Bocco na Mkude kwa mapenzi mema kwa wachezaji hao au wanawadhihaki.

Mapenzi mema kwao ni kwa sababu wameona umuhimu wao na ndio maana wamewaita na kuwaaga mbele ya halaiki ya wapenzi na mashabiki wa Simba ulimwenguni kote, najua Mkude aliipigania Simba tangu akicheza Simba B na baadaye timu ya wakubwa.

Lakini Bocco naye alicheza kwa mafanikio na ndio maana wakampa kitambaa cha unahodha, dhihaka inakuja kwa uongozi wa Simba kuwaaga sasa na si huko nyuma, Mkude aliachana na Simba msimu juzi, na Simba wamefanya matamasha mawili mpaka sasa.

Na Bocco aliachana na Simba msimu jana, na Simba wamefanya tamasha moja bila Bocco, Simba walipaswa kuwaaga wachezaji hao kwa wakati wao na si sasa, kuwaaga wachezaji hao ni dhihaka za waziwazj na si kuonesha mapenzi kama wenyewe wanavyodhani.

ALAMSIKI


Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa