Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Dili la Feitoto kwenda Simba limekufa kisa Yanga

Inasemekana dili la kiungo mshambuliaji wa Azam FC na timu ya taifa, Taifa Stars, Feisal Salum au Feitoto kujiunga na Simba linaelekea kufeli baada ya Afisa Hahari wa Azam FC, Zakharia Zaka Zakazi kuweka wazi kila kitu kwamba Simba haiwezi kumnunua.

"Azam haiwezi kumuuza Feisal kwenda Simba sababu Simba hiyo Pesa hawana, labda nikuambie mkataba wa Feisal unakipengele kama atauzwa kwenda Simba basi Yanga inabidi alipwe bilioni Moja (Yaani kwenye mkataba imetajwa kabisa Simba), sasa Simba atatoa shilingi ngapi ili Azam imlipe Yanga Bilion Moja na Azam abakiwe na Hela"
.
"Ndio maana nasema Simba hiyo Hela hawana labda waje na bilioni Mbili na nusu ili Yanga apewe bilioni Moja halafu Azam abakiwe na Bilion Moja na nusu sababu huwezi kuilipa Yanga Bilion Moja halafu sisi tubakiwe na Hela ndogo au tusipate Hela lazima sisi tupate Hela kubwa zaidi"
.
"Biashara ya Azam na Simba juu ya Feisal Haiwezi kufanyika yaani timu iliyonunuliwa kwa Bilion 20 unavyoona inaweza kutoa hiyo pesa ?, yaani timu nzima unaipata kwa 20B , Wakati hiyo Bilion 20 hapa Azam tumenunua mabasi mawili ndio maana hizo Tetesi zipo na zitaendelea kuwepo kuwa Feisal anaenda Simba lakini Hilo haliwezi kutokea"

Zaka zakazi amezungumza hayo kupitia Crown sports


Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa