Yanga yashikilia msimamo wake, hawachezi dabi

Bodi ya Ligi Kuu nchini Tanzania TPLB siku ya Jana ilifanya mawasiliano na Uongozi wa juu wa klabu ya Young Africans Sports Club kujadili masuala mbalimbali kuhusu mechi zilizosalia za kumaliza msimu.

Uongozi wa klabu ya Young Africans Sports Club 🔰 umeshikilia msimamo ule ule wa kusema hawautambui Mchezo wa tarehe 15/06/2025,wanatambua michezo miwili ya Ligi kuu ndio wamebakiza wao na Mchezo mmoja wa Fainali ya FA basi na si michezo mingine.

Mpaka kufikia Sasa hakuna muafaka wowote uliofikiwa baina ya pande hizo mbili kuhusu kutatua kitendawili Cha Mchezo huo ambao uliahiriahwa tarehe 08/03/2025 bila kufuatwa kwa kanuni.

Mazungumzo Bado yanaendelea ikishirikisha Viongozi wa Serikali pia