Klabu ya Wydad Casablanca imethibitisha kumsajili kiungo mshambuliaji, Stephanie Aziz Ki kwa mkataba wa miaka miwili akitokea Young Africans ya Tanzania akiungana na wachezaji wengine waliosajiliwa na klabu hiyo kama Nordin Amrabat na Hamza Hanouri.
Katika hatua nyingine Young Africans Sc imethibitisha kuwa nyota huyo raia wa Burkina Faso kuondoka klabuni hapo baada ya kutoa ‘Thank You’ kwa kinara huyo wa magoli kwenye Ligi Kuu bara msimu uliopita.