Rasmi, kocha wa Orlando atambulishwa Al Ahly

KOCHA Mspaniola, José Luis Riveiro jana alitambulishwa kuwa Kocha mpya wa Al Ahly ya Misri wiki mbili tu baada ya kuondoka Orlando Pirates ya Afrika Kusini.

Mara moja Riveiro anapewa jukumu la kwenda kuiongoza Al Ahly katika michuano ya Klabu Bingwa ya Dunia ya FIFA inayotarajiwa kufanyika nchini Marekani hivi karibuni.

Ahly, kati ya wawakilishi wenne wa Afrika pamoja na Wydad Athletics ya Morocco, Esparence ya Tunisia na Mamelodi Sundowns ya Afrika Kusini – ipo Kundi A pamoja na wenyeji, Inter Miami, Palmeiras ya Brazil na FC Porto ya Ureno.