Petro de Luanda yamtema straika wake mkongwe

Klabu ya Petro de Luanda wameachana rasmi na mshambuliaji wao mkongwe Adriano Nicolau, maarufu kwa jina la Yano.

Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 32 alirejea klabuni katikati mwa msimu wa 2024/25, na kucheza mechi 11 bila kufunga bao hata moja.