Manula kimeeleweka Yanga

Taarifa za kuaminika kutoka kwenye vyanzo vyetu vya habari kwamba mlinda mlango wa Simba SC Aishi Manula anaelekea kujiunga na watani zao Yanga SC kwenye dirisha kubwa lijalo.

Manula ingawa anahusishwa kurejea Azam FC, lakini si kweli-, Yanga wameingia kwenye rada ya Manula na tayari kipa huyo amekubali kutua Yanga kufungana na swahiba zake Jonas Mkude na Clatous Chama.

Manula atasaini mkataba wa miaka miwili, ingawa taarifa hazielezi mshahara wake na signing fee.