Kaizer Chiefs yakaribia kumsajili Diarra


Klabu ya Kaizer Chiefs Inataka kutumia uhusiano wao mzuri na klabu ya Young Africans sc ili kumpata Djigui Diarra.

Kaizer Chiefs wanatumia uhusiano huo kuwashawishi Young Africans ili wamuachie Djigui Diarra ili ajiunge kwenye klabu yao kwa dau watakalobkubaliana nao.

Mpaka sasa bado Young Africans hawajajibu chochote juu ya mpango huo uliokaa kimtego huku pia Uongozi wa klab hiyo ukipitia ofa zaidi 5 zilizotumwa kwao juu ya kumpata mlinda lango huyo bora ndani ya ligi kuu ya NBC.