Mwenyekiti wa Umoja wa Vilabu Afrika, Eng. Hersi Said anawapongeza sana Klabu ya RS Berkane kwa kubeba Ubingwa wa Kombe la Shirikisho la Afrika, siku ya jana Mei 25,2025, katika Uwanja wa New Amaan Complex, Zanzibar.
Berkane walibeba Ubingwa huo baada ya kuichapa Klabu ya Simba kwa jumla ya Mabao 3-1, Huku Klabu ya Simba ikiweka aibu ya ikipiga Shuti moja tu Lililolenga Lango [Shots On Target] ndani ya Dakika 180 za mechi za Fainali.
Aidha, Eng Hersi amesisitiza kuwa, Pongezi zake kwa Timu Afrika atazitoa kwa mabingwa tu na si vinginevyo.