Yanga na Kelvin Nashon kuteta upya


Klabu ya Young Africans SC mwanzoni mwa wiki ijayo itaanza mazungumzo rasmi tena na kiungo wa ulinzi kutoka Singida Black Stars, Kelvin Nashon ili kujiunga nao kuelekea msimu ujao

Kelvin Nashon anahitajika Young Africans SC ili kuongeza nguvu akishirikiana na kiungo wa ulinzi Khalid Aucho ambaye amekuwa akipata majeraha ya mara kwa mara, Young Africans inaamini Nashon ataongeza kitu kikubwa katika eneo la ulinzi kutokana na kipaji chake

Young Africans SC ilistisha mchakato wa kumsainisha Kelvin Nashon katika dirisha dogo la uhamisho kwakuwa klabu ilikuwa katika kipindi kigumu cha mwenendo wa matokeo uwanjani