Uwanja wa Uhuru zamani Taifa nao kufungwa taa

Uwanja wa Uhuru (zamani Taifa au shamba la bibi) uliopo jijini Dar es Salaam unaendelea kuboreshwa ili uwe uwanja wa kisasa wenye hadhi ya kutumika mashindano makubwa ya kimataifa.

Vile vile uwanja huo utaongezewa jukwaa, utawekewa viti vipya, utawekewa taa za kisasa na maboresho mengine yatakuwa sehemu ya kubadiliahia nguo pamoja na sehemu ya vyoo.