TFF, Bodi ya Ligi zafikishwa mahakamani

Shirikisho la Mpira Nchini Tanzania pamoja na Bodi ya Ligi Kuu Tanzania Wameitwa mbele ya Jaji wa Mahakama Kuu (masijala ndogo ya Dar Es Salaam) Mh. Jaji E. Mkwizu tarehe 2 Mei 2025 saa 1:30 asubuhi bila kukosa kwa ajili ya kusikiliza madai ya shabiki wa mpira wa miguu kutoka Iringa Mjini Dk. Samweli Marwa.
.
Kwenye shauri hilo TFF ndiye mdaiwa wa kwanza na Bodi ya Ligi ndiye mdaiwa wa pili na madai hayo yanahusiana na kuaihirishwa kwa mechi ya watani wa jadi tarehe 8 Machi 2025.