Shirikisho la Mpira Nchini Tanzania pamoja na Bodi ya Ligi Kuu Tanzania Wameitwa mbele ya Jaji wa Mahakama Kuu (masijala ndogo ya Dar Es Salaam) Mh. Jaji E. Mkwizu tarehe 2 Mei 2025 saa 1:30 asubuhi bila kukosa kwa ajili ya kusikiliza madai ya shabiki wa mpira wa miguu kutoka Iringa Mjini Dk. Samweli Marwa.
.
Kwenye shauri hilo TFF ndiye mdaiwa wa kwanza na Bodi ya Ligi ndiye mdaiwa wa pili na madai hayo yanahusiana na kuaihirishwa kwa mechi ya watani wa jadi tarehe 8 Machi 2025.