Straika wa Stellenbosch, Andre Ernest de Jong (jezi namba 18) raia wa New Zealand
amewapongeza Simba kutinga fainali na kuimwagia sifa zaidi safu ya ulinzi akimtaja Abdlurack kama ni moja ya walinzi alikuwa kikwazo kwake.
”Simba wana timu nzuri, safu yao ya ulinzi nzuri zaidi naweza kusema kwenye haya mashindano tangu mwanzo wao na RS Berkane walikuwa bora mno kuliko timu zote, yule jezi namba nne (Hamza) ni kati ya mabeki bora Afrika kwa sasa.”