Meneja wa Habari wa klabu ya Yanga, Ally Kamwe amethibitisha kuwa mshambuliaji, Clement Mzize atachezea Ligi Kuu Ufaransa msimu ujao ingawa hajabainisha ni timu gani kinara huyo wa magoli kwenye Ligi Kuu bara atachezea.
Ally Kamwe amebainisha kuwa Yanga Sc itapata bilioni 5 kwa mauzo ha nyota huyo ingawa ameshindwa kuitaja timu timu inayomtaka
"Siwezi kuitaja timu lakini kuna mazungumzo na Timu ya Ufaransa, Yanga tunapata bilioni 5, msimu ujao Mzize atakuwa Ligi Kuu Ufaransa kama kuna timu ina bilioni 5 ilete,” — Ali Kamwe