Yanga yaichabanga bila huruma Mashujaa FC 5-0

Mabingwa watetezi wa Ligi Kuu bara Yanga SC jioni ya leo imezidi kujikita kileleni mwa msimamo baada ya kuichabanga bila huruma Mashujaa FC mabao 5-0 katika uwanja wa Lake Tanganyika mjini Kigoma.

Kwa ushindi huo Yanga imefikisha pointi 55 ikiwa imecheza mechi 21 ikiwaacha watani zao kwenye nafasi ya pili na pointi 50 wakiwa wamecheza mechi 19.

Mabao ya Yanga leo yamefungwa na kiungo Mkenya, Duke Ooga Abuya dakika ya 31, mshambuliaji Mzimbabwe, Prince Dube Mpumelelo dakika ya 48, viungo — Mganda Khalid Aucho dakika ya 53 na Mzambia, Clatous Chota Chama mawili, dakika ya 74 na 83.

Kesho Simba SC watacheza na Azam FC katika uwanja wa Mkapa jijini Dar es Salaam mechi ambayo inatajwa kuwa ngumu na kali


Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI