Sowah, Rupia watupia, Singida Black Stars ikiifunga Mashujaa 3-0

Wenyeji Singida Black Stars leo imeendeleza wimbi la ushindi baada ya kuichabanga Mashujaa FC mabao 3-0.

Mabao ya Singida Black Stars yamefungwa na washambuliaji, Mghana Jonathan Sowah mawili, dakika ya 57 kwa penalti na dakika ya 60, wakati lingine limefungwa na Mkenya Elvis Rupia dakika ya 90.

Goli la Rupia limenifanya afikishe mabao 9 na kuendeleza harakati zake za kuibuka mfungaji bora