Singida Black Stars yamuongeza benchini Melis Medo

Klabu ya Singida Black Stars imetangaza kumuongeza Melis Medo kama kocha msaidizi na mshauri wa benchi la ufundi wa timu hiyo, atakayeshirikiana na makocha Juan Magro, Muhibu Kanu chini ya kocha mkuu David Ouma.

Mabadiliko hayo ni muendelezo wa marekebisho kwenye benchi lao la ufundi, ambapo hivi karibuni walimuongeza Juan Magro kama kocha msaidizi.