TIMU ya Pamba Jiji ya jijini Mwanza jioni ya leo imewabana mbavu wenyeji wao Singida Black Stars baada ya kutoka nayo sare ya mabao 2-2 uwanja wa Liti mjini Singida.
Mabao ya Singida Black Stars yamefungwa na washambuliaji, Muivory Coast, N'guessan Serge Archange Pokou dakika ya 10 na Mghana, Jonathan Sowah kwa penalti dakika ya 32, wakati ya Pamba yote yamefungwa na mshambuliaji Mkenya, Mathew Tegisi Momanyi dakika ya 28 na 47.