Baba yake Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI Mohamed Mchengerwa, Alhaj Omary Mchengerwa amefariki leo Alfajiri akiwa kwenye Ibada ya Umrah huko Makka.
Kwa mujibu wa taarifa ya Familia ya Mchengerwa, Mzee Omary atazikwa leo huko huko Makka.
Ifuatayo ni Ratiba ya Ibada ya Visomo vitakavyoongozwa na Mufti wa Tanzania Dkt Zuberi Bin Ali wa Mbwana nyumbani kwa Waziri Mchengerwa, Masaki Dar es Salaam.
LEO: TAREHE 24 FEBRUARI 2025
Dua ya Kisomo itafanyika nyumbani kwa Mhe. Mohamed Mchengerwa Masaki saa 10 Alasiri
KESHO TAREHE: 25 FEBRUARI 2025
Dua ya kisomo itafanyika Jimboni Rufiji
KESHO KUTWA TAREHE: 26 FEBRUARI 2025
Dua itafanyika nyumbani kwake Marehemu Alhaj Omary Mchengerwa Yombo.