Milioni 300 kuvunja mkataba wa Nangu wa JKT Tanzania kwenda Yanga


Inaelezwa Yanga inasaka beki mwingine wa kati ili kusaidiana na nahodha Bakari Mwamnyeto, Ibrahim Bacca na Dickson Job, na kiwangio kilichoonyeshwa na beki wa JKT Tanzania Wilson Nangu kimewavutia mabosi hao na kupisha hodi jeshini.

Chanzo cha ndani kutoka JKT Tanzania kinasema; “Ni kweli Yanga imekuja kuomba iuziwe beki huyo hivyo imepewa dau la kuvunja mkataba ambalo ni Sh300 milioni, kisha itaendelea na mazungumzo na mchezaji mwenyewe kukubaliana mambo ya mshahara na ishu nyingine za kimasilahi.”

Wilson Nangu