Kinda Mtanzania anayecheza ligi daraja la kwanza nchini Zambia Maurice Sinchone (18) ameisaidia timu yake ya Trident FC kupata alama 1 leo baada ya kufunga bao dhidi ya Konkola Blades kwenye mchezo wa ligi daraja la kwanza nchini humo.
Hivi sio Vipaji ambavyo tunaweza kuviacha vipotee, Mchezaji anacheza nje ya nchi akiwa na umri mdogo kama Mourice, inabidi tumkumbatie kwa namna yeyote ile na kumuweka kwenye mipango kama Taifa, hata AFCON ya U20 anastahili kujumuishwa.