Habari mbaya kwa Bares katupiwa virago Mashujaa

Taarifa za awali zinaarifu ya kwamba Klabu ya Mashujaa imemfuta kazi kocha wake Abdallah Mohammed Baresi mara baada ya kupoteza mchezo dhidi ya Singida Black Stars na hii ni kutokana na mfululizo wa matokeo mabaya ya klabu hiyo katika ligi kuu Tanzania bara.

Mashujaa ilipoteza mchezo dhidi ya Yanga SC kwa mabao 5-0 katika ardhi yake ya mjini Kigoma, Bares amekuwa na mwendelezo mbaya tangu kuanza kwa mzunguko wa pili