Timu ya Fountain Gate imepata ushindi wake wa kwanza baada ya kupoteza kwa muda mrefu, ilipoifunga Tanzania Prisons bao 1-0.
Bao la mkwaju wa penalti la Amos Charles dakika ya 27 limeipa Fountain Gate ushindi wa 1-0 dhidi ya Tanzania Prisons katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara leo Uwanja wa Tanzanite Kwaraa mjini Babati mkoani Manyara.