Kwa mujibu wa watu wakaribu wa Msani wa Muziki wa Bongo fleva Lava lava Tayari Ameshavunja mkataba na lebo yake ilikuwa ikimsimamia ili kuanza kujitegemea Akiwa Kama Solo Artist kilichobaki kwa Sasa Ni kukamilisha malipo ya uvunjaji mkataba ambapo kwa Sasa wameshalipa Asilimia kadhaa na wanategemea kukamilisha malipo yaliyobaki ili kukabidhiwa hatimiliki za digital platform zake na Mambo mengine .kumbuka hii sio Mara ya kwanza kwa wasani kutoka Wcb kuvunja mikataba hii imefanyika kwa Rich mavoko, Harmonize, Rayvanny Sasa Ni lavalava
SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.
