Ruka hadi kwenye maudhui makuu

KOCHA POWER DYNAMOS AIGWAYA SIMBA

Baada ya kutinga Raundi ya Kwanza ya mechi za Ligi ya Mabingwa Afrika kwa kuing’oa African Stars ya Namibia kwa faida ya bao la ugenini na kutambua sasa itavaana na Simba SC, Kocha Mkuu wa Power Dynamos ya Zambia, Mwenya Chipepo ameonekana kuingiwa ubaridi akisema anawafahamu vizuri wapinzani wao ili na sasa wanajipanga upya kuvunja rekodi ya Wekundu hao.

Dynamos imetinga hatua hiyo baada ya awali kufungwa 2-1 ugenini kisha jumamozi (Agosti 26) ikalipa kisasi nyumbani kwa kushinda 1-0 na kufanya matokeo ya mwisho kuwa 2-2 na kupenya kwa kanuni ya faida ya bao la ugenini na itavaana na Simba SC mwezi ujao ikiwa ni mwezi mmoja tangu zikutane kwenye pambano la kirafiki la kimataifa kwenye Tamasha la Simba Day na miamba hiyo ya Zambia kulala 2-0 Kwa Mkapa.

Akizungumza kutoka nchini Zambia, Chipepo alisema sio wageni kwa Simba SC, wanaifahamu vizuri kuanzia ubora wao wa timu na rekodi zao kwenye michuano hiyo, hivyo wanajipanga ili kuivunja, kwani kwa miaka ya hivi karibuni, Simba SC imekuwa ikifuzu makundi na kukwamia Robo Fainali ya Michuano ya CAF.

Simba SC ni timu nzuri na ina wachezaji wengi wenye zoefu, tumecheza nao mechi ya kirafiki Agosti 6 mwaka huu tukafungwa mabao 2-0, kilikuwa ni kipimo sahihi kwetu tumesawazisha makosa na kufanikiwa kutinga hatua ya kwanza,” amesema Chipepo na kuongeza

“Kukutana nao sio habari mpya kwetu tulitarajia kitu hiki tutaingia kwa kuwaheshinu kutokana na rekodi yao nzuri dhidi yetu na ubora wao kwenye michuano hii, malengo yetu ni kutinga hatua ya makundi tutapambana kuhakikisha lengo hilo linatimia.”

Chipepo amesema wanafahamu ubora wa kikosi cha Simba SC ulipo na udhaifu wao hivyo watapambana kuhakikisha wanafanya jitihadi za kuwadhibiti ili waweze kuweka heshima katika mechi za mashindano.#

Akizungumzia ubora wa mchezaji mmoja mmoja ndani ya kikosi cha Simba SC amesema kila mchezaji aliye ndani ya kikosi cha timu hiyo ni bora na ndio maana kasajiliwa, hivyo hawezi kuzungumzia mchezaji mmoja mmoja.

“Naheshimu kila mchezaji na wachezaji wangu mara baada ya kutinga hatua inayofuata tulikaa pamoja na kukumbushana aina ya timu tunayoenda kukutana nayo.”


Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa