Rasmi, Tarimba awatuliza Yondani, Kessy, Yanga

Na Salum Fikiri Jr. Dar es Salaam

Aliyekuwa mwenyekiti wa kamati maalumu ya mpito ya klabu ya Yanga , Abbas Tarimba amefanikiwa katika Juhudi zake za kumzuia beki Kelvin Yondani asisajiliwe na klabu ya Simba  mara baada ya kufikia makubaliano kwa beki huyo kuendelea kuitumikia klabu hiyo .

Jana tena Tarimba alifanya mazungumzo na Kelvin Yondani na mchezaji huyo kukubali Kuongeza kandarasi mpya klabuni hapo .

Inasemekana klabu ya Simba SC ilikuwa inamuwinda kwa hudi na Uvumba beki huyo lakini Jitihada zao zilishindwa kutokana na makubaliano kutofikiwa baina ya Simba SC na Kelvin Yondani .

Tarimba ambaye amesisitiza anataka kujiondoa katika kamati maalumu ya mpito ya klabu ya Yanga pia amefikia makubaliano na Hassan Kessy ili aweze kubaki klabuni hapo .

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI