Wenger amtetea Sanchez kukataa kupima

Mkufunzi wa Arsenal, Arsenel Wenger amemtetea mchezaji wake wa zamani Alexis Sanchez aliyejiunga na mashetani wekundu, Manchester United kwa kukataa vipimo.

Sanchez amekataa kupima afya kama anatumia madawa ya kuongeza nguvu ama hatumii, raia huyo wa Chile alikataa kupimwa baada ya kutakiwa na madaktari.

Katika taarifa yake. meneja wa Arsenal, Arsenel Wenger amedai hakuna ulazima wowote wa kupima kwani Sanchez hatumii dawa hizo na anajiamini kwa kile anachokiamini

Alexis Sanchez amekataa kupima afya