MKUDE ATIMKIA TENA SOUTH

Na Mwandishi Wetu, DAR ES SALAAM

KIUNGO mkabaji na fundi Jonas Gerald Mkude ametimka tena katika kikosi cha Simba na kuelekea nchini Afrika Kusini kujaribu bahati yake nyingine ya kucheza soka la kulipwa.

Taarifa ambazo zimethibitishwa zinasema kiungo huyo ameondoka Simba wiki iliyopita kuelekea Afrika Kusini kufanya majaribio ya kucheza soka la kulipwa katika klabu moja inayoshiriki Ligi kuu nchini humo.

Hii ni mara ya pili kwa kiungo huyo mkabaji kwenda kufanya majaribio nchini Afrika Kusini, Awali alijiunga na Bidvest Wits lakini alishindwa, na sasa ameenda tena kujaribu bahati yake.

Mchezaji huyo hakuwemo kwenye kikosi cha wachezaji 29 wa Simba walioingia kambini mjini Morogoro, Simba imeweka kambi Morogoro ikiwa tayari kabisa kujiandaa na msimu ujao wa Ligi kuu bara

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI