MFUNGAJI BORA ZIMBABWE ATUA AZAM KUMRITHI BOCCO

Na Mrisho  Hassan, DAR ES SALAAM

MSHAMBULIAJI anayeongoza kwa mabao Bruce Kangwa wa timu ya Ligi kuu nchini Zimbabwe ya Highlanders, amewasili nchinj leo tayari kabisa kujiunga na Azam FC inayonolewa na makocha raia wa Hispania.

Kangwa ambaye pia ni mchezaji wa timu ya taifa ya Zimbabwe na anatoka kwenye klabu kongwe na kubwa nchini humo ametua leo akiwa tayari kurithi nafasi ya nahodha John Rafael Bocco ambaye ameshaonyeshwa mlango wa kutokea.

Mshambuliaji huyo aliyetupia magoli 20 kwenye ligi ya nchi hiyo inasemekana ni mkali kuliko mshambuliaji wa Yanga Donald Ngoma ambaye naye ni raia wa Zimbabwe

Bruce Kangwa akiwasili leo Airport

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI