KIBADEN AONDOLEWA UKOCHA JKT RUVU

Na Saida Salum, DAR ES SALAAM

TIMU ya JKT Ruvu imeamua kuachana na kocha wake mkuu Abdallah King Kibaden Mputa na kumpa mikoba hiyo mchezaji wa zamani wa Mlandege Malale Hamsini.

Kibaden aliyekuwa akiinoa timu hiyo na kuikoa isishuke daraja, atakuwa mkurugenzi wa ufundi na atakuwa akidili zaidi na timu za vijana, kwa mujibu wa mtoa taarifa hizi anasema kuwa Malale Hamsini ataweza kukinoa kikosi hicho na kufanya vizuri msimu ujao.

Kibaden pia amewahi kuzinoa Simba, Manyema, Ashanti, Kagera Sugar na timu ya taifa, Taifa Stars

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI