Ruka hadi kwenye maudhui makuu

YANGA WATAKIWA KUFANYA UCHAGUZI JUNI 5

Na Mwandishi Wetu  DAR EA SALAAM

SHIRIKISHO la soka nchini TFF limeitaka klabu ya Yanga kuitisha uchaguzi wake ifikapo Juni 5 kulingana na agizo lilikotolewa na BMT na wizara.

Akizungumza na waandishi wa habari, mwenyekiti wa kamati ya uchaguzi TFF, Aloyce Komba amesema mchakato mzima wa uchaguzi wa Yanga utakuwa ndani ya siku 33.

Komba ambaye pia ni Wakili, amesema mchakato rasmi wa uchaguzi wa Yanga utaanza Mei 3, 2016, Komba amesema jukumu lao TFF kusimamia na kuhakikisha uchaguzi unafanyika katika hali ya demokrasia.

Wakili Komba ameongeza kuwa kamati yake itatangaza mchakato mzima wa uchaguzi huo wa Yanga na kubandika tangazo kwenye mbao za matangazo na kutangaza nafasi zitakazogombaniwa.

Mei 4-9, 2016 kuchukua fomuza wagombea na mwisho wa kurudisha kwa wagombea, Mei 10, 2016 kamati ya uchaguzi TFF itakaa kikao cha mchujo wa awali wa wagombea na kuandika barua za kuwajulisha wagombea juu ya mchujo huo wa awali.

Mei 11, 2016 kamati ya uchaguzi ya TFF itachapisha na kubandika kwenye mbao za matangazo orodha ya awali ya wagombea, Mei 12-13_ 2016 kipindi cha kupokea na kuweka pingamizi kwa wagombea wote.

Mei 14-15, 2016 kamati ya uchaguzi TFF itapitia pingamizi zote na kufanya usajili wa wagombea, Mei 16, 2016 kamati ya uchaguzi TFF itatangaza na kubandika kwenye mbao za matangazo matokeo ya awali ya usahili.

Mei 17, 2016 Sekretalieti kuwasilisha masuala ya kimaadili kwenye kamati ya maadili ya TFF, Mei 18-19, 2016 kamati ya maadili ya TFF itappkea na kusikiliza na kutolea maamuzi ya kamati maadili.

Ratiba kamili ya uchaguzi inaonyesha kuwa Mei 20, 2016 kamati ya maadili itatangaza maamuzi ya masuala ya kimaadili, Mei 21-22 kipindi cha kukata rufaa, Mei 23, kamati ya maadili TFF itasikiliza rufaa.

Mei 24, kamati ya rufaa na maadili itatoa maamuzi ya rufaa, Mei 25 na 26 kipindi cha kukata rufaa kwa kamati ya uchaguzi dhidi ya kamati ya TFF, Mei 27-28 muda wa kusikiliza rufaa na Mei 29 kamati ya uchaguzi itatangaza maamuzi ya rufaa.

Mei 30 kamati ya uchaguzi itachapisha orodha ya majina ya wagombea na kubandikwa kwenye mbao za matangazo, Mei 31 na Juni 4, kipindi cha kampeni kwa wagombea na Juni 5 ni siku ya uchaguzi mkuu wa klabu ya Yanga

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa