MICHANO: ZAY B MWANADADA GAIDI ALIYENASWA KIZEMBE NA SISTA P

Na Mkola Man, TANGA

Yap...yap....yap. michano ya leo inamchana mwanahip hop wa kwanza wa kike hapa bongo Zainabu Lipangile maarufu Zay B aliyetamba na wimbo wake uitwao 'Gado' aliomshirikisha Inspekta Haroun 'Babu' na remix yake alimshirikisha Juma Nature.

Zay B mwanadada gaidi, gaidi aliyekamatwa na Sister P ambaye alikuwa pandikizi la kumshusha Zay B, alichokosea Zay B wakati anakimbizwa, alisimama akijifanya yeye ni gaidi.

Laiti kama angekimbia asingekamatwa na Sister P na ndio maana waswahili husema ukikimbizwa usigeuke nyuma, utajikwaa, ushauri wangu kwa rapa Zay B kipaji hakizeeki kisha ajue kutofautisha kukaa na kuchuchumaa.

Mashabiki wake bado wapo, Michano ya Mkola Man lengo ni kujenga na si kubomoa, Tukutane wiki ijayo siku kama ya leo, je unataka tumchane nani 0715281223

Zay B mwanadada gaidi aliyekamatwa kirahisi na Sister P

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI