Carlos Tevez amerejea Boca Juniors



Mshambulizi wa Argentina na washindi wapili katika kombe la mabingwa mwaka huu Juventus Carlos Tevez amerejea katika klabu yake ya zamani ya Boca Juniors.

Tevez, 31, alianzia huko huko Argentina katika Boca Juniors kabla ya kuondoka mwaka wa 2004 kwa ziara iliyomweka barani ulaya kwa kipindi cha miaka 9.

Tevez ambaye alitamba Uingereza katika vilabu vya Manchester United, Manchester City na West Ham kabla ya kuhamia Italia kujiunga na mabingwa msimu huu Juventus .


Tevez alifunga mabao 20 katika ligi kuu ya Serie A.
Tevez aliisaidia Argentina kuilaza Colombia katika robo fainali ya Copa America

Kulikuwa na uvumi wake kurejea Uingereza katika dirisha la uhamisho katika msimu wa joto ambapo jina lake lilihusishwa na uhamisho kwenda Liverpool, Atletico Madrid ama Paris St-Germain.

Hatma yake huko Italia ilikuwa imeshabainika baada ya Juventus kusajili huduma za mshambulizi wa Atletico Mario Mandzukic.

Tevez akijaribu kupiga mbele ya mabeki wa timu pinzani

Boca Juniors walithibitisha uhamisho huo licha ya kuwa Tevez alikuwa akipasha joto benchi katika robo fainali ya Copa America Argentina ilipokuwa ikikabiliana na Colombia.

Ilikuwa sadfa kwani punde tu baada ya Boca kutangaza uhamisho huo,Tevez aliingia uwanjani kama mchezaji wa akiba na akafunga penalti iliyoiwezesha Argentina kufuzu kwa nusu fainali ya Copa America.

Tevez, alishinda mataji mawili ya ligi nchini Uingereza na mawili nchini Italia.

Rais wa Boca,Daniel Angelici alisema''ni siku njema sana kuwa Carlos Tevez anarejea nyumbani,nina hakika kuwa ataimarisha ushindani wetu katika klabu ya Boca.

Tevez, alishinda mataji mawili ya ligi nchini Uingereza na mawili nchini Italia.

Tevez akiwa na Messi katika jezi ya timu ya taifa ya Argentina

Alifunga mabao 38 katika mechi 110 alipoichezea Boca mara ya kwanza.

Wakati huo aliisaidia kutwaa taji la ligi kuu mwaka wa 2003 mbali na kutawazwa mchezaji bora katika ligi hiyo ya Marekani ya kusini kwa miaka mitatu mfululizo.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

STAA WETU: JEREMIA JUMA MTOTO WA JUMA MGUNDA ALIYEIKACHA SIMBA NA KUENDELEA NA UASKARI