Ruka hadi kwenye maudhui makuu

PHIRI AAHIDI UBINGWA MSIMBAZI, MAXIMO AMTUNISHIA MISULI

Wakati Kocha Mkuu wa Simba, Mzambia Patrick Phiri akidai ubingwa bila kuifunga Yanga hauna raha, Marcio Maximo ametamba kutumia kikosi mseto cha wakongwe na chipukizi kwenye Ligi Kuu Bara iliyopangwa kuanza Septemba 20, mwaka huu.

Akizungumza na gazeti hili kabla ya kuondoka kuelekea visiwani Zanzibar mwishoni mwa wiki ambako Simba imeweka kambi ya kujiandaa na msimu mpya, Phiri alisema moja ya mikakati aliyojiwekea ni kuhakikisha anatwaa ubingwa wa Ligi Kuu Bara lakini hautanoga bila kuifunga Yanga.

"Moja ya mikakati niliyojiwekea ni kuhakikisha Simba inatwaa ubingwa wa ligi ikiwa chini yangu, lakini nitafurahi zaidi nikitwaa ubingwa na kuifunga Yanga," alisema Phiri.


Alisema msimu huu amejipanga kuhakikisha anairejesha raha iliyopotea kwa muda mrefu Msimbazi kwa kuwa mikakati yake ya kwanza ni klabu hiyo kufanya vizuri katika mechi za mzunguko wa wa kwanza na badaye kuhitimisha kwa kutwaa ubingwa.

Phiri ambaye awali katika msimu wa 2004/05 aliipa Simba ubingwa kabla ya ule wa 2009/10 kuhitimisha kwa kutwaa ubingwa bila kupoteza mechi, alisema amejipanga kutoa mazoezi ya makini katika idara zote ili kuwaweka sawa wachezaji wake kabla ya kuanza kwa ligi hiyo.

Mzambia huyo aliondoka jijini Dar es Salaam jana kuelekea Zanzibar kuungana na kikosi cha timu hiyo kwa ajili ya kuendelea na mazoezi ya kujiandaa na Ligi Kuu ya Bara.

Wakati Phiri akieleza hayo, Maximo alisema kikosi chake kipo kamili na mazoezi ya kujiandaa na Ligi Kuu ya Bara na kwamba mazoezi ambayo wameshafanya yamekamilika na kilichobaki ni kurekebisha kasoro ndogo ndogo.

"Timu ipo kamili kwa sasa, imebaki kiasi kidogo kukamilisha mazoezi tayari kwa kuanza Ligi Kuu," alisema Maximo.
Alisema amejipanga kuhakikisha Yanga inafanya vizuri katika michuano hiyo na kutwaa ubingwa ambao kwa sasa unashikiliwa na Azam FC ya jijini Dar es Salaam.

Simba na Yanga zote zimeweka kambi visiwani Zanzibar kwa ajili ya kujiandaa na Ligi Kuu Bara huku mabingwa watetezi Azam FC wakiitumia michuano ya Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati (Kombe la Kagame) kujiwinda na Ligi Kuu.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa