Ruka hadi kwenye maudhui makuu

YANGA YAIENDEA SIMBA BAGAMOYO

Klabu  ya Yanga ambayo ilirejea jijini Dar es Salaam jana ikitokea Moshi ilikocheza mechi ya kirafiki dhidi ya Panone FC wakati ikiwa njiani kutokea Arusha, imeweka kambi yake Kawe Beach na imeelezwa kwamba huenda wakahamia Bagamoyo mkoani Pwani kwa ajili ya mechi yao ya kukamilisha ratiba ya Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara dhidi ya mahasimu wao Simba.

Ofisa Habari wa Yanga, Baraka Kizuguto, alisema jana kwamba aulizwe kuhusu kambi ya timu hiyo akishafika Dar es Salaam akitokea Moshi, lakini mara baada ya kutua walikwenda moja kwa moja Kawe Beach na habari kutoka ndani zilisema kwamba kambi hiyo inaweza ikahamia Bagamoyo.


Hata hivyo, mshambuliaji wa kimataifa kutoka Uganda, Emmanuel Okwi, yuko katika hatihati ya kujiunga na kambi hiyo kutokana na kuhitaji alipwe fedha zake za usajili anazoidai klabu hiyo.

Okwi aliyejiunga na Yanga Desemba mwaka jana anaidai klabu hiyo dola za Marekani 50,000 na imeelezwa kwamba juzi alikataa kupokea kiasi cha dola za Marekani 20,000 ambazo ilikuwa atanguliziwe.

Chanzo cha gazeti hili kilieleza kuwa Okwi aliambiwa apokee dola 20,000 ili arejee kundini kujiandaa na mechi dhidi ya Simba Jumamosi lakini Mganda huyo alikataa.

Habari zaidi kutoka Yanga zilieleza kuwa aliyekuwa mwenyekiti wa klabu hiyo, Francis Kifukwe, alimtaka Okwi akubali kiasi hicho na kuahidiwa kumaliziwa fedha nyingine zilizobakia mara baada ya viongozi wengine wa juu wa Yanga watakaporejea nchini.

Rafiki wa karibu wa Okwi aliliambia gazeti hili kwamba mshambuliaji huyo amegoma kupokea malipo hayo kwa mafungu ili kujiepusha na suala na kuja kusotea kiasi kilichobakia.

"Mechi hiyo ya Simba Jumamosi ndiyo ya mwisho, anajua asipolipwa sasa itakula kwake", alisema rafiki huyo ambaye alikuwa naye tangu alipokuwa anaichezea Simba.

Okwi hapatikani katika simu zake za mkononi na inaelezwa pia hata mahali anapolala amekuwa anabadilisha kulingana na atakavyojisikia siku hiyo.

Yanga tayari imeshavuliwa ubingwa na Azam FC na inachotaka katika mechi hiyo ya funga dimba ni kulinda heshima kwa wanachama na wapenzi wa timu hiyo.

Kwa kumaliza katika nafasi ya pili, Yanga itaiwakilisha nchi mashindano ya kimataifa ya Kombe la Shirikisho mapema mwakani.

Kocha wa timu hiyo, Mholanzi Hans van der Pluijm, alisema kuwa atawatumia wachezaji waliofanya mazoezi tu kwa ajili ya mechi hiyo ya Jumamosi.

Alisema kuwa hataki kuzungumzia mchezaji asiyekuwa pamoja na timu kwa sababu za kiutawala.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa