Ruka hadi kwenye maudhui makuu

UHURU SELEMAN AINYIMA UBINGWA SIMBA

Uhuru Suleiman amesema timu yake ya Simba ina mazingira magumu ya kutwaa ubingwa kutokana na ushindani mkali iliopo kwenye ligi kuu ya Bara  ugumu uliopo katika duru la pili.

Lakini, kiungo huyo amesema, Simba bado ina nafasi ya kutwaa taji hilo kama itarekebisha makosa yaliyojitokeza nyuma na kufanya vizuri katika mechi zilizosalia.

Akizungumza na Nipashe katikati ya wiki, Uhuru ambaye hakuambatana na Simba jijini Mbeya ambako ilitoka sare ya 1-1 na Mbeya City Jumamosi iliyopita alisema ligi imekuwa gumu kutokana na timu kukamiana na ndiyo maana timu yake haifanyi vema.

"Ligi katika duru la pili imekuwa ngumu mno," alisema Uhuru nyota wa zamani wa Mtibwa Sugar na Coastal Union.


"Timu zinakamia na zinafukuzia pointi tatu."

Hata hivyo alisema pamoja na Simba kuonekana kuyumba katika mechi zake za karibuni, bado ina nafasi ya kuwa bingwa kwa sababu kuna mechi nyingi kabla ya msimu kufungwa.

Simba iliyopoteza pointi saba katika mechi zake tatu zilizopita kwa kupata sare mbili dhidi ya Mtibwa Sugar na Mbeya City na kulala kwa Mgambo JKT ipo nafasi ya nne kwenye msimamo, ikiwa pointi nne nyuma ya viongozi Azam wenye mechi mbili mkononi juu.

Mabingwa hao wa zamani kesho wataikabili JKT Ruvu iliyo katika nafasi za katikati za msimamo na ambayo mwalimu wake mpya kocha msaidizi wa zamani wa Yanga, Fred Felix 'Minziro' alipokelewa na kipigo cha 6-0 kutoka kwa Prisons katikati ya wiki.
 

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa