Ruka hadi kwenye maudhui makuu

OKWI KUONGOZA MAUAJI YANGA LEO

Yanga leo inashuka kwenye Uwanja wa Taifa kucheza na Ruvu Shooting huku kocha mkuu wa timu hiyo, Hans Van der Pluijm akipanga kumtumia mshambuliaji Emmanuel Okwi kwa mara ya kwanza kwenye michezo ya ligi kuu ya Bara.

Okwi hajaichezea timu hiyo mchezo wowote wa ligi tangu alipotua timu hiyo katika dirisha dogo la Januari kutokana na utata uliokuwapo kwenye usajili wake.

Afisa Habari wa klabu hiyo, Baraka Kizuguto, alisema Pluijm anaweza akamtumia Okwi leo kulingana na mahitaji yake.

"Suala la Okwi kucheza au kutocheza hilo lipo mikononi mwa kocha kulingana na kikosi chake atakachokipanga kesho," alisema Kizuguto kwa sababu "kocha kwa sasa yupo huru kumtumia na kutokana na mazoezi ya leo (jana) asubuhi ni wazi atamtumia."


Aidha, Kizuguto alisema Pluijm anajivunia ushirikiano na umoja wa wachezaji wake wanaoendelea kuuonyesha klabuni hapo.

Mashabiki wa klabu hiyo wana hamu kubwa ya kumuona kwenye ligi mshambuliaji Mganda huyo ambaye alifanya vizuri akiwa na klabu yake ya zamani ya Simba hapa nchini kabla ya kuuzwa kwa klabu ya Etoel du Sahel ya Tunisia miezi 13 iliyopita.

Yanga inavaana na Ruvu Shooting ikitokea kwenye mashindano ya kimataifa ambapo iliitoa Komorozine ya Comoro kwa jumla ya magoli 12-2 kwenye raundi ya awali ya Ligi ya Klabu Bingwa Afrika.

Van Pluijm alisema michezo ya ligi kuu ni sehemu ya maandalizi kabla ya kuvaana na mabingwa watetezi Al-Ahly ya Misri Jumamosi ijayo katika mechi ya raundi ya kwanza ya michuano hiyo ya Afrika.

Mbali na kutumia ligi kuu ya Bara kama mazoezi ya maandalizi, timu hiyo ilimtuma kocha msaidizi Charles Mkwasa Misri kushuhudia mchezo wa Super Cup kati ya Alhy na mabingwa wa Kombe la Shirikisho la klabu za Afrika CS Sfaxien ya Tunisia.

Mkwasa aliyerejea jana, alitumwa kuwasoma mabingwa mara nane hao Afrika kabla ya kuvaana nao Machi mosi.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa