Ruka hadi kwenye maudhui makuu

SHOMARI KAPOMBE HATIHATI KUTUA YANGA AU AZAM.

Beki wa zamani wa Simba ya jijini Dar es Salaam, Shomary Kapombe, amesema yeye sasa ni mchezaji huru na yuko tayari kufanya mazungumzo na klabu yoyote ya ndani na nje ya nchi ambayo itahitaji huduma yake.

Kapombe ambaye kwa sasa yuko hapa nchini, alikuwa akilelewa kisoka Ufaransa katika Klabu ya AS Cannes akiichezea kwa mkopo kwa lengo la kutumia nafasi hiyo kupata uzoefu wa ligi ya nchi hiyo kabla ya kutafutiwa soko.

Simba ilimtoa beki huyo na kumpeleka Ufaransa kupitia wakala wa mchezaji huyo.

Akizungumza juzi jijini, Kapombe, alisema baada ya Klabu ya AS Cannes kusitisha malipo yake ya mshahara na posho, aliamua kuikacha na kutorejea huko kuendelea na timu hiyo inayoshiriki Ligi Daraja la nne.


Kapombe alisema bado ndoto zake za kucheza Ulaya hazijapotea lakini ataangalia maslahi kwanza endapo atapata timu yoyote ya kuichezea hapa nchini. "Mimi niko huru, nilikuwa kwetu Morogoro mzima wala siumwi," alisema beki huyo wa timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) juzi mara baada ya mechi ya kirafiki kati ya Simba na Mtibwa Sugar iliyochezwa Uwanja wa Taifa.

Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Simba, Zacharia Hanspope, alisema hivi karibuni kuwa Kapombe ni mali ya wakala na wakala huyo ndiye anawajibika kwa matatizo yoyote yatakayomkuta mchezaji huyo.

Hanspope alisema wao walichokubaliana na wakala huyo ambaye ni raia wa Ufaransa ni kuhakikisha Kapombe anapata timu ya kucheza huko Ulaya itakayomlipa vizuri na endapo atauzwa rasmi, klabu hiyo ya Msimbazi itapokea malipo ya asilimia 40. Tayari habari ambazo viongozi wa Yanga na Azam wamekataa kuthibitisha ni kwamba wanamhitaji beki huyo ambaye anacheza zaidi ya namba tatu uwanjani.

Mwaka jana Simba ilishuhudia mshambuliaji wake raia wa Uganda, Emmanuel Okwi, akijiunga na wapinzani wao Yanga kiulaini huku wao wakiendelea kuidai timu ya Etoile du Sahel ya Tunisia Dola za Marekani 300,000.

Kama ilivyokuwa kwa Okwi, Kapombe kabla ya kuondoka alikuwa na mkataba na Simba hivyo klabu hiyo ilihitajika kulipwa kabla ya nyota huyo kuingia mkataba na klabu hiyo ya Ufaransa.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa