Ruka hadi kwenye maudhui makuu

MSANII WA BONGOFLEVA MATATANI KWA DAWA ZA KULEVYA TANGA.

MSANII wa muziki wa kjizazi kipya anayevuma sana kwenye mitandao ya kijamii kwa sasa Christopher Mhenga maarufu Mkola Man (Pichani) ameingia kwenye mzozo mwingine safari hii akihusishwa na matumizi ya dawa za kulevya na kupelekea kutengwa na baadhi ya marafiki Mambo Uwanjani imeelezwa.

Akizungumza na mtandao huu mara baada ya kuulizwa na mwandishi wa habari hizi kama kweli alifumwa akijidunga dawa hizo za kulevya, Mkola Man alikanusha vikali na kudai yeye atumii kabisa dawa hizo isipokuwa sigara tu.

'Mimi situmii kabisa dawa za kulevya nashangaa kusikia taarifa hizo kuwa natumia dawa, unajua tangia nimeanza kupata umaarufu kupitia wimbo wangu wa Kilevi changu  vyombo vya habari hasa mitandao ya kijamii vimekuwa vikiniandika tofauti', aliendelea kulalamika.


Alidai kuwa hivi karibuni alihusishwa na kujiunga na dini ya kishetani ya freemason ambapo imefikia hatua familia yake imemtenga, ameendelea kusema kuwa jamii isimfikirie vibaya na yeye ni mtu safi anayehitaji ushirikiano na watu ili kutimiza malengo.

Amedai anapigana kwa nguvu zote kupinga dawa za kulevya na anashangaa kuona anatajwa kati ya watu wanaotumia wakati yeye anayapinga, ingawa ni msanii na kazi yake kuelimisha jamii bila shaka atasimama mstari wa mbele kupinga, aidha Mkola Man amepanga kukanusha vikali juu ya kuhusika kwake na kundi l,a freemason

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa