Ruka hadi kwenye maudhui makuu

MAKALA: DINO MANYUTI, NYOTA MPYA BONGOFLEVA ANAYETAMBA NA TAM TAM.

Na Exipedito Mataruma

Kizazi kipya ndani ya bongofleva, apania na wimbo wake Tam tamNi kijana mdogo anayetokea kukonga nyoyo za mashabiki wa muziki wa kizazi kipya kwa sasa na wimbo wake wa Tam tam ambao umeanza kupata wafuasi wengi.

Kutamba kwa wimbo wake huo kunaweza kumfanya afikie dhamila yake ya kujulikana na kuweza kupata mafanikio kama ilivyo kwa nyota wengine wa muziki huo wa kizazi kipya.

Bila shaka mbuyu ulianza kama mchicha, hata masupa staa wa sasa kama Naseeb Abdul maarufu Diamond Plutinum, Ommy Dimpoz, Rich Mavoko, Ay na wengineo hawakuanza kujulikana ghafra, walitumia muda wao mpaka kufahamika na sasa wanafaidi matunda ya muziki.

Abdalah Ramadhani Manyuti a.k.a 'D Sina shaka' (Pichani) ameanza kupata unafuu baada ya kusota kwa muda mrefu kwenye muziki huo bila mafanikio yoyote, Kijana huyo anaweza kufikia nyendo za wakali wengine wa muziki huo.


Akizungumza na mwandishi wa habari hizi Manyuti alisema kwamba alianza muziki tangia mwaka 2005, 'Nilianza muziki toka mwaka 2005 ila rasmi nilianza kurekodi mwaka 2007 'Pasu kwa Pasu studio Ludigo ndio prodyuza wa kwanza kunitengenezea wimbo', alisema na kuongeza.

'Nikafanya ngoma studio moja inaitwa Kama kawa rekord kwa Marco Chali alikua prodyuza wangu wa pili, ikaja mwaka 2009 nikafanya ngoma studio nyingine inaitwa Kazi One Record ilikuwa mwaka 2010 ndio nikawa rebo Burn record iliyo chini yake Sheddy Clever.

Mwaka 2013 mwezi wa 12 nikakutana na Sabi Sam ambaye ndiye bosi wangu wa sasa tukafungua studio inayoitwa Rash Records tukatengeneza ngoma ya kwanza iitwayo Tam tam, prodyuza anaitwa Naroh na ndio ngoma ambayo ipo redioni kwa sasa', alisema na kuongeza.

'Tumeshafanya video, video yenyewe nikali sana imefanywa na Raymond Kasogaa 'The dream videos'  malengo yangU ni kuufanya muziki wangu uwe wa kimataifa nahitaji kufanya mapinduzi makubwa kwenye muziki wetu wa bongo fleva, sasa hivi nipo chini ya Rash Ent chini ya mkurugenzi Sabi Sam na meneja maneno Mr Project watanzania wakae mkao wa kula kwani nimepania kufanya makubwa sana kwenye muziki wetu wa Tanzania', alimaliza Manyuti.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa